• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mamlaka za Serikali za Mitaa
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Zaidi ya Kaya 2,900 Kunufaika na Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (PSSN II) Geita MJI

Posted on: April 15th, 2021

Imeelezwa kuwa, jumla ya Tshs.167, 972,000 zitazinufaisha kaya 2,919 zinazoendelea kunufaika na Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini ndani ya Halmashauri ya Mji Geita ikiwa ni kipindi cha tatu cha uhawilishaji fedha tangu kuanza kwa mpango wa kunusuru kaya masikini awamu ya pili TASAF III- PSSN II.

Hayo yamebainishwa Aprili 14, 2021 na Mratibu wa TASAF Mkoa wa Geita Bw. Elikana Haruni alipokuwa katika ziara ya kufanya mikutano ya uamsho katika mitaa ya Geita Mji iliyopo kwenye kwenye mpango huo wakati wa uhawilishaji wa fedha huku akihimiza ufikiwaji wa malengo ya mpango, kuwahimiza wanufaika hao juu ya utekelezaji wa masharti ya mpango, kujisajili ili kupokea fedha kwa njia ya simu, lakini vilevile kusikiliza kero na changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo walengwa.

Bw. Haruni amewaeleza wanufaika hao kuwa, inawapasa kuzingatia masharti ya elimu na afya kila wapatapo fedha hizo ili kuhakikisha zinawasaidia watoto wanaowalea na kuwatimizia mahitaji yao kupitia fedha hizo kisha kutumia kiasi bakia kujiimarisha kiuchumi ili kuondokana na sifa ya umasikini uliokithiri. Vilevile, wanufaika hao wamesisitizwa juu ya kusajili namba zao za simu ili waweze kupokea fedha hizo kwa njia ya simu ya mkononi ili kuondoa usumbufu wakati wa kupokea huku wakionywa kutumia simu zao kukopea fedha mitandaoni na baadaye kuona kama fedha hizo hazijawekwa baada ya kukatwa kwenye mitandao ya simu.

“nimeona niwakumbushe juu ya masharti ya mpango, kuwahamasisha ambao hamjasajili namba zenu kwaajili ya kupokea fedha kwenye simu lakini pia muepuke kutoa namba zenu za siri mkiwapa vijana wenu ambao wengine hutumia namba zenu kukopea fedha, na endapo zikatumwa basi zitakatwa na mitandao husika nanyi mtapata fedha pungufu, hivyo muwe makini” alisema bw Haruni.

Akihitimisha, mratibu Haruni ameonya wapokeaji wa fedha wenye tabia ya kuwatenga wenza wao akisisitiza kuwa, TASAF huwaleta wenza karibu na isiwe chanzo cha familia kugombana kisa fedha wanazozipokea kupitia mpango.

Walengwa hao katika nyakati tofauti, wamemshukuru mratibu huyo kwa namna ambavyo amekuwa akiwatembelea na kutoa ufafanuzi juu ya mambo mbalimbali ambapo walengwa hao wameahidi kuendelea kuzitumia fedha hizo kama ilivyokusudiwa.

Itakumbukwa kuwa, mpango huu wa Kunusuru Kaya Masikini kipindi cha pili ulizinduliwa jijini Dodoma Februari, 2020 na aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli baada ya Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini awamu ya kwanza kukamilika.

Jumla ya mitaa 5 ya Mkolani, Katoma, Msalala Road, Mbugani na Uwanja imetembelewa na mratibu huyo.




Matangazo

  • WALIOCHAGULIWA MAFUNZO YA KILIMO KUPITIA PROGRAMU YA BBT-YIA FEBRUARI, 2023 March 16, 2023
  • KARIBU UPATE FOMU YA USHIRIKI KWENYE MAOENSHO YA TANO YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI 2022 September 11, 2022
  • THE 5TH TANZANIA MINERALS TRADE FAIR (TMTF) PARTICIPATION FORM September 12, 2022
  • THE 5TH TANZANIA MINERALS TRADE FAIR (TMTF) SPONSORSHIP PACKAGES September 11, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Zaidi ya Milioni 293 za RUWASA Zawatua Ndoo Kichwani Wananchi 10,448 Nzera&Bugando

    March 19, 2023
  • Tupeleke Mafunzo ya Mfumo wa PVMIS Ngazi za Vituo- Asema Dkt.Mkapa

    March 16, 2023
  • Mfumo wa PVMIS Kurahisisha Upatikanaji wa Bidhaa za Afya-Geita

    March 14, 2023
  • Mfumo wa PVMIS Kurahisisha Upatikanaji wa Bidhaa za Afya-Geita

    March 14, 2023
  • Tazama Zote

Video

Mwaliko Jukwaa la Fursa za Biashara Mkoani Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa