• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Zaidi ya 600 Wakutana Geita Kujadili Mkakati wa Kuboresha Lishe, RC Shigela Azindua Mwongozo wa Lishe Shuleni

Posted on: December 8th, 2023

Na Boaz Mazigo - Geita RS

Katika kutekeleza maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan, Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe.Martine Shigela amekutana na kufanya kikao cha kimkakati na wataalam mbalimbali wa Halmashauri za Mkoa wa Geita kwa lengo la kujadili na kuweka mikakati ya kuboresha lishe na kuondoa Udumavu kwa watoto hasa wenye umri chini ya miaka 5, jambo ambalo limekuwa likichangia hata ufaulu duni wa wanafunzi kutokana na historia ya makuzi na vyakula walivyokuwa wakivitumia.

Kikao hicho kiliketi Desemba 8, 2023 siku moja kabla ya siku ya maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara kilichofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Nyankumbu iliyopo mjini Geita ambapo pamoja na mjadala uliofanyika, iliazimiwa kuwa suala la Lishe liwe ni Agenda ya kudumu kwenye vikao mbalimbali ili kuendelea kupata matokeo chanya.


Akizungumza kabla na baada ya kuhitimisha kikao kazi hicho, mkuu wa mkoa wa Geita Mhe.Martine Shigela alisema ni muhimu kuzingatia maazimio ya kikao hicho ikiwemo kila Halmashauri kuhakikisha fedha iliyotengwa kwenye bajeti kwa ajili ya lishe inatolewa yote lakini pia kuhakikisha zinatenga shilingi 1,000 kwa kila mtoto kwenye eneo la lishe.

"kwanza niwapongeze viongozi wa Halmashauri kwa kuwezesha wataalam hawa mbalimbali kufika kwenye kikao hiku muhimu. Suala la lishe si la idara ya afya pekee, tushirikiane sote kwa pamoja ili tuweze kufanikiwa. Maazimio tuliyoweka, viongozi ngazi ya wilaya na Halmashauri muyasimamie", alisema RC Shigela

Vilevile RC Shigela alisema, ni vyema watumishi wa Umma kuwa na umoja na mshikamano na kwamba kwa kufanya hivyo ni rahisi kupata mafanikio, kisha kuhitimisha kwa kuzindua kitabu cha Mpango wa Utekelezaji wa Mwongozo wa Kitaifa wa Utoaji wa Huduma ya Chakula na Lishe kwa Wanafunzi wa Elimumsingi.

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita Nicholas Kasendamila alisema," ninakupongeza sana RC Shigela kwa uongozi wako, unaipenda kazi yako. Na muhimu kwa watumishi ni kwamba, ili tufanikiwe ni muhimu tupendane, tuthaminiane, tujaliane na tuheshimiane, tusitegesheane. Pia, nisisitize juu ya uadilifu kwani unaleta mafanikio hadi kufanikisha utekelezaji wa Ilani ya CCM"

Kwa upande mwingine, kaimu katibu tawala mkoa Dkt.Elfas Msenya alisema atahakikisha maelekezo na maazimio yanawafikia wahusika na yanatekelezwa.

Mganga mkuu wa mkoa Dkt. Omari Sukari alitumia fursa hiyo kuwakumbusha wataalam wa afya kutoa elimu kwa wananchi kuchukua tahadhari kufuatia ugonjwa wa kipindupindu ulioripotiwa mkoa jirani na kwamba endapo wataona mtu mwenye dalili zozote zinazoashiria ugonjwa huo, basi hatua zichukuliwa kwa wakati na endapo watapatikana wagonjwa watibiwe kule walipo na wasihamishwe kwani kwa kufanya hivyo kutapelekea kusambaza ugonjwa na kwamba atasimamia watumishi wa afya kuenenda kwa weredi

Dkt. Sukari aliongeza kuwa, matarajio ya Mhe.Rais.Dkt.Samia Suluhu Hassan ni kutoa huduma bora kwa wananchi, hivyo mtumishi mzembe hatovumiliwa na pia aliwakumbusha watumishi wa sekta ya afya kuwa makini na matumizi ya mitandao ya kijamii wakizingatia maadili ili kuepusha taharuki wanaporusha mambo yao binafsi mtandaoni.

Kikaokazi hicho cha kimkakati kiha viongozi wa CCM Mkoa na wilaya, Kamati ya Usalama Mkoa, Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Geita, Wenyeviti wa Halmashauri zote za Geita, Makatibu Tawala Wilaya Wote, Wakurugenzi Watendaji Halmashauri zote za Geita, Wenyeviti kamati za kudumu za huduma za jamii za Halmashauri, timu ya afya mkoa, waweka hazina, maafisa utumishi, maafisa mipango, maafisa elimu, waganga wakuu, waratibu elimu kata, watendaji wa kata, maafisa lishe, maafisa Tarawa, viongozi wa vyama rafiki vya siasa pamoja na wadau wa Maendeleo




Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa