• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Watumishi wa Umma Waonywa Kutoichonganisha Serikali na Wananchi Wake

Posted on: July 30th, 2019

Watumishi wa Umma ndani ya mkoa wa geita wamekumbushwa juu ya misingi mbalimbali ya utumishi ndani ya serikali huku wakionywa kuhusu kuepuka kuichonganisha serikali na wananchi wake kupitia huduma wanazozitoa.

Hayo yameelezwa na Mratibu wa Utawala wa Utumishi wa Umma kutoka Ofisi ya Rais-Ikulu Bw. Francis Mang’ira Julai 29, 2019 katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa wakati akiwasilisha maelekezo kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi kwa watumishi wa sekretarieti ya mkoa, hospitali ya mkoa na wakuu wa taasisi za umma mkoani hapa.

 “kila mtumishi wa umma kwa nafasi yako hakikisha hauichonganishi serikali na wananchi kwa kuhakikisha kila mwananchi anapofika kupata huduma katika ofisi za umma anapokelewa, anasikilizwa na kuhakikisha anaelekezwa sehemu husika hata kama shida yake si ya ofisi uliyopo”. Amesema Bw.Mang’ira.

Ameendelea kueleza kuwa, watumishi wa umma hawatakiwi kuchanganya masuala ya siasa wanapotekeleza majukumu yao ili kuepuka upendeleo, uonevu, usumbufu n.k huku akisisitiza juu ya kumhudumia mwananchi katika ubora, usahihi, haki, bila upendeleo na ubaguzi.

Pamoja na hayo, watumishi pia wame elekezwa kuhakikisha wanafanya kazi na kuepuka majungu  na kutoingilia majukumu ya wenzao wakihimizwa kila mmoja kuhakikisha anakuwa na malengo na mikakati ya utekelezaji wa kazi zake katika kuhakikisha huduma stahiki zinamfikia mwananchi huku akikemea tabia ya viongozi wa ngazi za chini wanaouza huduma kwa wananchi ambazo tayari serikali imekwisha kuzilipia.

Kwa upande wake Bw.Abdallah Mnongane ambaye ni Mratibu Msaidizi wa Utawala wa Utumishi wa Umma Kutoka Ofisi ya Rais-Ikulu amesisitiza juu ya uzingatiaji wa SHERIA, TARATIBU na KANUNI (STK), bila kusahau miongozo na maelekezo mbalimbali yanayotolewa na viongozi.

Bw. Mnongane amehimiza juu ya idara, vitengo na taasisi kuwa na utamaduni wa kufanya vikao hata mara mbili kwa mwezi ili viwezeshe kutoa mrejesho wa utendaji, vilevile kuwa kama chombo cha kuibua changamoto na kero za watumishi na si kupeleka kero zao nje ya ofisi.

Kuheshimu madaraka, kuzingatia maadili ya utendaji kazi katika utumishi wa umma, nidhamu, kushughulikia malalamiko ni sehemu ya yaliyoelekezwa na Bw. Mnongane akisema watumishi ni vyema kuyazingatia.

Maelekezo hayo yanaendelea kutolewa kwa watumishi wa umma ndani ya mkoa wa geita ambapo hadi sasa tayari yamefikishwa kwa watumishi walioko wilaya ya Geita, Chato, Nyang’hwale na Bukombe.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa