• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mamlaka za Serikali za Mitaa
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

“Tanzania Bila UKIMWI Inawezekana”. Asema Mhe.Toufiq

Posted on: March 2nd, 2022

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI, TB, Madawa ya Kulevya na Magonjwa Yasiyoambukiza kwa pamoja wameiambia jamii ya Tanzania kupitia mkoa wa Geita kuwa, Tanzania bila maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI inawezekana kutokana jitihada mbalimbali zinazoendelea kufanywa na Serikali ya Tanzania inayoongozwa na kiongozi shupavu Mhe.Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hayo yameelezwa Mosi Machi, 2022 katika ukumbi wa Mwl.Julius Nyerere EPZ-Mjini Geita wakati wa kuahirisha kikao cha kamati hiyo baada ya kukutana na Konga la vijana na watu wazima wanaoishi na virusi vya UKIMWI ndani ya Halmashauri ya Mji Geita lililotanguliwa na ziara ya wajumbe wa kamati hiyo katika mkoa wa Geita kupitia Mgodi wa GGM, yenye lengo la kufatilia afua mbalimbali katika kupambana na magonjwa hayo, huku wakitoa shime kwa mkoa kuongeza juhudi katika mapambano ikiwemo kutafuta wadau wa sekta ya afya ili kwenda kwa kasi zaidi.

Akiongea wakati wa kuahirisha kikao hicho, mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe.Fatma Toufiq alisema, “ofisi ya mkuu wa mkoa wa Geita tunawapongeza kwa jitihada mnazozifanya kwa mfano Halmshauri ya Mji walivyotueleza kuokoa watoto wengi wanaozaliwa na wazazi wenye maambukizi ya VVU lakini wao wakatoka salama, hii inaonesha elimu inatolewa hongereni sana. Pia niwasihi, elimu hii iendelee na tuwatumie vijana wa rika sawa ili tuweze kufikisha ujumbe kwa wengi na kwa kufanya hivyo Tanzania bila UKIMWI inawezekana”

Mhe.Toufiq aliendelea kusema kuwa, “kipekee niwapongeze GGM, NACOPHA na TACAIDS kwa namna ambavyo nanyi mmekuwa msaada mkubwa kwenye mapambambano dhidi ya VVU. Nikifikiri jinsi leo ilivyo rahisi mtu kujisema waziwazi kuwa ameathirika ninaona jitihada ni kubwa hivyo niwaombe kazi iendelee".

Kwa upande mwingine Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Geita ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe.Dkt.Sophia Mjema alisema, “kwanza niwakaribisheni sana Geita lakini mfahamu kuwa kama mkoa tumefarijika na ujio wenu, hatuna shaka nanyi ukizingatia mnafuatilia utekelezaji wa Ilani ya chama tawala CCM, hivyo tunaamini ujio wenu utaleta mabadiliko kwa wananchi kwakuwa nao wanaona fedha nyingi zinazotolewa na serikali yetu pendwa, hivyo karibuni sana”.

Naye Naibu Waziri wa Afya Mhe.Dkt.Godwin Mollel (Mb) alianza kwa kumpongeza Mganga Mkuu Mkoa wa Geita Dkt.Japhet Simeo pamoja na GGM akisema GGM ni ya Kuigwa na kuwaasa watumishi wa serikali kufanya kazi kwa weledi mkubwa na kuishauri kamati hiyo kuwa na pendekezo la kuwepo kamati itakayohusika na Sayansi na Uvumbuzi ili kuisaidia serikali na wananchi katika mazingira inapoibuka mijadala na hoja kuhusu wagonjwa wengi wa saratani kutoka kanda ya ziwa na sababu kuonekana ni shughuli za madini huku akiahidi kushughulikia changamoto zilizojitokeza zinazoikabili sekta ya afya.

Vilevile, Naibu Waziri wa Madini Mhe. Steven Kiruswa (Mb) alitoa pongezi za wizara kwa Mgodi wa GGM kwa kuwa wadau muhimu kwa serikali na kuahidi kushughulikia changamoto na ufafanuzi wa masuala mbalimbali kwa kuwa na siku maalumu ya kufanya kikao na mgodi ili kuja na majibu juu ya masuala mbalimbali yaliyoulizwa na wajumbe wa kamati.

Katika kuhitimisha, wajumbe mbalimbali akiwemo Mhe.Abdul-hafar Idrissa (Mb) alisema, ni muhimu kwa wabunge kuwa na kampeni ya wabunge vijana kuhamasisha zoezi la upimaji ili kuwahamasisha vijana wengine kupima afya zao na kujilinda lakini pia Mhe.Esther Malleko (Mb) akawapongeza NACOPHA na kuomba ziwepo jitihada za pamoja kulisaidia kundi la vijana kupitia mapambano dhidi ya VVU, TB na Madawa ya Kulevya na Magonjwa Yasiyoambukiza ili kuokoa nguvu kazi ya taifa.

Geita ya Dhahabu, Utajiri na Heshima


Boazi Mazigo

Afisa Habari

Geita RS



Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2022 YATOKA January 29, 2023
  • KARIBU UPATE FOMU YA USHIRIKI KWENYE MAOENSHO YA TANO YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI 2022 September 11, 2022
  • THE 5TH TANZANIA MINERALS TRADE FAIR (TMTF) PARTICIPATION FORM September 12, 2022
  • THE 5TH TANZANIA MINERALS TRADE FAIR (TMTF) SPONSORSHIP PACKAGES September 11, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Shigela Asisitiza Mambo Matatu, Kiapo cha Ma DC Geita

    January 30, 2023
  • RC Shigela Asisitiza Mambo Matatu, Kiapo cha Ma DC Geita

    January 30, 2023
  • “Mgogoro wa Shambani Humalizwa Shambani”. Asema RC Shigela.

    December 29, 2022
  • RC Shigela Akabidhi Zawadi za Rais Samia

    October 16, 2022
  • Tazama Zote

Video

Mwaliko Jukwaa la Fursa za Biashara Mkoani Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa