• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Serikali Kuendelea Kuboresha Uchimbaji Mdogo

Posted on: October 18th, 2024


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa. Dkt. Samia Suluhu amesema kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kujenga mazingira rafiki katika kuwawezesha wachimbaji wadogo mikopo na mitambo ya uchimbaji katika makundi mbalimbali wanayoyaunda.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ametoa kauli hiyo hivi karibuni mjini Geita alipokuwa akizungumza na wananchi waliojitokeza kwa wingi kwenye hafla ya ufungaji rasmi wa Maonesho ya saba ya Teknolojia ya Madini iliyofanyika katika viwanja vya EPZ Bombambili Geita mjini.

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameeleza kuwa wachimbaji wadogo wamechangia asilimia 40 katika sekta ya madini kutoka asilimia 10 hivyo makundi ya mbalimbali kama kundi la wanawake na vijana watapatiwa mashine za kuchorongea ili waweze kuchimba kisasa na uhakika tofauti na uchimbaji wa kubahatisha.


“Napenda kutoa wito kwa wachimbaji wote wa madini kuacha tabia ya utoroshaji wa madini au biashara zisizo halali badala yake pelekeni dhahabu zenu na aina nyingine za madini katika masoko maalum yaliyotengwa na Serikali maalum kwa shughuli ya uuzaji na ununuzi wa madini ili muweze kuuza madini hayo kwa bei elekezi na kusaidia kukuza uchumi wa Nchi.

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametumia fursa hiyo kuupongeza uongozi wa Umoja wa wachimbaji wadogo (FEMATA) kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuwaunganisha wachimbaji wadogo Nchini na kushughulikia changamoto mbalimbali zinazowakabili.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela ameeleza kuwa jumla ya wachimbaji wadogo 3,301 wamepatiwa leseni ikiwa ni utekelezaji wa agizo alilolitoa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa ziara yake mkoani humo Oktoba 2022.

Mhe. Shigela ameongeza kuwa uchumi wa Mkoa wa Geita unategemea hasa wachimbaji wadogo ambao kwa mwaka 2023 walizalisha kilo za Dhahabu Zaidi ya elfu 16 zenye thamani ya shilingi trilioni mbili. Pia ameeleza mipango ya uboreshwaji wa uwanja wa Maonesho EPZ Bombambili kuwa wa kisasa kwa kujenga majengo ya kudumu na kupewa hadhi ya kuitwa uwanja wa Maonesho wa Dkt. Samia Suluhu Hassan.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa