• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RC GEITA: Nitoe wito kwa wazazi kuhakikisha watoto wetu wanaenda shuleni waachane na utoro

Posted on: December 7th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Rosemary Senyamule amewataka wazazi Mkoani Geita kusimamia watoto na kuhakikisha wanakwenda shule na kuachana na tabia ya utoro kwani serikali imedhamiria kuwapatia elimu bora.

Mhe. Mkuu wa Mkoa ametoa wito huo leo tarehe 07 desemba, 2021 wakati akizungumza na wananchi baada ya kuweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa madarasa 6 shule ya Sekondari Nyamigota kwa Tshs. Milioni 120 za Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Uviko 19.

"Nitoe wito kwa wazazi kuhakikisha watoto wetu wanaenda shuleni waachane na utoro nasi tutachukua hatua kwa wazazi ambao watoto wao watakua watoro na walimu mfundishe kwa bidii." Mkuu wa Mkoa.

"Tumeondoa ujinga na maradhi na tunaona Mhe. Rais wa awamu ya sita amesema anataka watoto wote wapate elimu, hayo ni mapinduzi yanaendelea kufanywa na serikali ya awamu ya sita na ndio maana watoto 405 tunawapokea katika kata hii moja pekee ifikapo mwezi januari 2022," amesisitiza Mkuu wa Mkoa.

Aidha, Mhe. Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa wananchi kuadhimisha miaka 60 ya Uhuru kwa kujituma kufanya kazi kwa bidii kwa maendeleo ya Taifa."Sababu ya serikali kuboresha huduma zake kama umeme, barabara, Maji na Elimu ni kuwataka wananchi wake wajiletee maendeleo, Miaka 60 ya Uhuru si wakati wa kulala usingizi na si wakati wa kubweteka hivyo tutumie fursa, Usalama na amani ya nchi ni wakati wa kujituma na kujiletea maendeleo hivyo tutimize wajibu wetu." Amesema.

Vilevile, Mhe. Mkuu wa Mkoa amekagua Ujenzi wa Madarasa kwenye shule ya Sekondari Lutozo na Shantamine pamoja na kupanda miti ambapo ameagiza Ukamilishaji wa kazi ndogo ndogo zilizobakia na utunzwaji wa miti iliyopandwa. "Hatua mliyofikia ni hatua ya matumanini kwani kazi zilizobaki ni ndogo na tutafanikisha tarehe 15 Disemba, 2021 aliyoagiza waziri wa TAMISEMl tutakamilisha."

"Kupanda mti sio kazi kazi ni kuitunza, nawaomba muitunze miti hii kwani miti inaleta uhai, miti inaleta mvua na hewa safi na kila mmoja aitunze kama kumbukumbu ya miaka 60 ya Uhuru, tukumbuke kuwa wanaopanda miti ni wachache lakkini wanaotumia kunufaika nayo ni wengi." Mhe. Senyamule.

"Miaka 60 ya Uhuru na 59 ya Jamhuri, nchi hii iko salama na tunaishi kwa upendo na hii ndio Tanzania iliyoundwa na wazee wetu na usione vyaelea ujue imeundwa, na hapa nataka niwaambie wazazi wote kuwa Serikali itaendelea kutoa Elimu Bure nchini." Amesema Ndugu Ally Rajab Kwa niaba ya CCM wilaya ya Geita.

Halmashauri ya Wilaya ya Geita inatekeleza ujenzi wa madarasa 347 ya Sekondari na 5 kwenye shule shikizi na kufanya jumla ya Madarasa 352 chini ya Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Uviko 19 kwa Jumla ya Tshs. Bilioni 6.9.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa