• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mamlaka za Serikali za Mitaa
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RAS Geita Akutana na Watumishi wa Umma Kujadili Changamoto- Wiki ya Utumishi wa Umma

Posted on: June 18th, 2019

Ikiwa ni mwendelezo wa Wiki ya Utumishi wa Umma nchini, Katibu Tawala Mkoa wa Geita Denis Bandisa amekutana na kuzungumza na watumishi wa umma ngazi ya sekretarieti ya mkoa akisikiliza changamoto zinazowakumba, ikiwa ni mojawapo ya programu zilizoandaliwa katika maadhimisho ya wiki hii muhimu kwa watumishi, kikao kilichofanyika Juni 18, 2019 katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa geita.

Akielezea umuhimu wa wiki ya utumishi wa umma, Bandisa amewashukuru watumishi hao kwa namna ambavyo wameonesha ushirikiano kwa kipindi chote ambacho ameendelea kutumikia katika nafasi hiyo, huku akiwataka kuendelea kushikamana, kushirikiana, kufanya kazi kama wamoja pamoja na kuwa na mahusiano mazuri baina ya watumishi katika kutekeleza majukumu ya kiutumishi.

“ninashukuru sana kwa ushirikiano wenu, utumishi bila kupendana na kushirikiana hauwezi kusogea. Nimewaita tuongee changamoto, tujadiliane, tutatue, ili twende mbele na hivi ndivyo tunavyoadhimisha wiki hii lakini pia tuongeze juhudi”, alisema Bandisa

Bandisa aliendelea kusema kuwa, katika wiki hii atazunguka na kuongea na watumishi wa umma walioko kila halmashauri ndani ya mkoa huu kwa lengo la kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili ili kuweka mazingira rafiki ya kufanyia kazi, kisha kupokea maoni na changamoto za watumishi hao.

Akiongea kabla ya kumkaribisha mwenyekiti wa kikao hicho, katibu tawala msaidizi, Utawala na Rasilimali Watu Herman Matemu amesema, pamoja na kikao hicho, wiki hii kutakua na programu mbalimbali ikiwemo mafunzo ya ujazaji wa fomu za Opras katika kuboresha utendaji kazi wa watumishi.

Deborah Zella, David Makabila, Masoud Biteyamanga, Abdallah Mfaume, dkt Japhet Siemeo na Felix Mabula ni baadhi ya watumishi waliotoa maoni na michango mbalimbali katika kikao hicho wakiwakilisha watumishi wengine huku wengi wao wakigusia juu ya maslahi ya watumishi kufanyiwa kazi kwa wakati.

Halikadhalika katika kikao hicho, Mkuu wa kitengo cha TEHAMA ofisi ya mkuu wa mkoa wa geita Lazarus Moshi akatumia nafasi hiyo kuwashauri watumishi kuendelea kuwa na matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA kwa kulinda siri za ofisi huku akiahidi kuboresha mawasiliano ya kieletroniki ndani ya ofisi hiyo.

Kikao kilihitimishwa kwa kuwaacha watumishi katika ari mpya ya kufanya kazi, huku wakiahidi kuendeleza Juhudi, mshikano, ushirikiano na kusaidiana ili kwa pamoja kuwatumikia wananchi.


Matangazo

  • MATOEKEO YA KIDATO CHA SITA YATANGAZWA July 05, 2022
  • HOTUBA YA BAJETI YA NCHI KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2023 June 01, 2022
  • BAJETI YA MKOA June 28, 2022
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan Amemuapisha Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Rosemary Staki Senyamule Tarehe 19 Mei 2021 May 19, 2021
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • “Watumishi Jipangeni Kuwahudumia Wananchi, Ofisi Tunayo”- Asema RC Shigela

    August 06, 2022
  • “Sensa ni Kipaumbele Chetu Hadi Agosti 23, 2022”. Asema RC Shigella.

    August 05, 2022
  • “Sensa ni Kipaumbele Chetu Hadi Agosti 23, 2022”. Asema RC Shigella.

    August 05, 2022
  • Sensa si Mzaha, ni Maisha ya Watu, Tujiandae Kuhesabiwa-Asema RC Senyamule

    July 28, 2022
  • Tazama Zote

Video

Mwaliko Jukwaa la Fursa za Biashara Mkoani Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa