• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mamlaka za Serikali za Mitaa
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Nyalwanzaja Wapongzwa Ujenzi wa Sekondari ya Ghorofa, KM 14 Zapunguzwa kuifuata Elimu

Posted on: April 15th, 2021

Mhandisi Robert Gabriel, Mkuu wa Mkoa wa Geita afurahishwa na Ujenzi wa Shule ya Ghorofa ya Sekondari Nyalwanzaja Wilayani Geita ambayo kwa uwepo wake itaondoa adha kwa wanafunzi kutembea zaidi ya KM 14 kufuata Elimu hiyo, mradi unaoambatana na Ujenzi wa nyumba pacha ya walimu pamoja na matundu kumi ya vyoo na kugharimu zaidi ya Milioni 200.

Mhe. Mkuu wa Mkoa amesema hayo tarehe 12, 04, 2021 wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Nyalwanzaja mara baada ya kuweka jiwe la Msingi kwenye Mradi wa Ujenzi wa shule ya Sekondari Nyalwanzaja iliyoasisiwa ujenzi wake na wananchi.

"Hii itakua shule ya kwanza ya Ghorofa Geita, nawapongeza sana wananchi wa hapa maana maendeleo haya ni ninyi ndio mmeyachochea." Amesema Mkuu wa Mkoa.

Akizungumza na viongozi wa shule mpya ya Sekondari Buyagu yenye wanafunzi wa kidato cha kwanza pekee, Mhe. Mkuu wa Mkoa amesema ameridhishwa na matumizi ya fedha kwenye Mradi huo ambao hadi sasa umetumia fedha.Tshs. Milioni 90 na tayari wameshajenga madarasa 5, Ofisi 2 za walimu na matundu 8 ya vyoo na madarasa mengine mawili yakiwa kwenye hatua ya boma.

Aidha, Mhe. Mkuu wa Mkoa amewataka watendaji kwenye ngazi zote kujituma na kufanya kazi kwa weledi ili kuhakikisha wanatatua kero za wananchi na kukamilisha Miradi kwa wakati huku akitoa rai kukamilisha ujenzi wa shule ya Sekondari Nyalwanzaja ukamilike ifikapo mwenzi Mei 2021.

Vilevile, Mhe. Mkuu wa Mkoa ametembelea Ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Nyabulolo na Kamena ambazo ziko kwenye hatua za mwisho kukamilisha na ameagiza ukamilishaji wa haraka ili huduma za mama na mtoto, wagonjwa wa nje, Afya ya uzazi, ziweze kutolewa kuanzia mwezi mei mwaka huu huku akitolea mfano wa unafuu mkubwa utaoletwa kwa zaidi ya wananchi 7786 kutoka Kamena waliokua wakitembea kilomita 15 kwenda kupata huduma hiyo.

Shule ya Sekondari Nyamalimbe yenye ziada ya vyumba vya madarasa 7 imemfurahisha Mhe. Mkuu wa Mkoa na amewapongeza uongozi wa Wilaya hiyo pamoja na shule kwa kujitoa kuhakikisha wanaondoa kero ya vyumba vya madarasa. Aidha, ameagiza ukamilishaji wa utengenezaji wa viti na meza vichache kwenye shule hiyo ili kuwapa wanafunzi mazingira mazuri ya kujifunzia.

Wakati huohuo Mhe. Mkuu wa Mkoa amesikitishwa na upungufu wa samani hasa kwenye maabara na upungufu mkubwa wa nyumba za walimu na mabweni ya wanafunzi wa kike kwenye Shule ya Sekondari Butobela na kaagiza ndani ya mwezi viongozi kwenye kata hiyo na wilaya waketi na kupate mkakati wa kukamilisha miundombinu hiyo.

Aidha, amehuzunishwa na matokeo dhaifu ya kitaaluma kwa kidato cha nne kwenye shule hiyo iliyoshika nafasi ya mwisho 2020 na akaagiza uthibiti ubora wa shule kumpatia taarifa ya kina ya sababu ya kufeli na akaagiza Katibu Tawala wa Mkoa kubadilisha Mkuu wa shule hiyo Mara moja kwa kushindwa kumudu majukumu yake.

"Yaani shule inakua ya mwisho mara mbili, ukipambana unabaki palepale, hii sio sawa Kaimu Katibu Tawala lete Mkuu wa shule mwingine apa ndani ya siku tatu awe amepatikana."

Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Geita amehitimisha siku ya kwanza ya ziara yake wilayani Geita kwa kutembelea shule za Sekondari za Nyamalimbe, Butobela na Bukoli.


Matangazo

  • WALIOCHAGULIWA MAFUNZO YA KILIMO KUPITIA PROGRAMU YA BBT-YIA FEBRUARI, 2023 March 16, 2023
  • KARIBU UPATE FOMU YA USHIRIKI KWENYE MAOENSHO YA TANO YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI 2022 September 11, 2022
  • THE 5TH TANZANIA MINERALS TRADE FAIR (TMTF) PARTICIPATION FORM September 12, 2022
  • THE 5TH TANZANIA MINERALS TRADE FAIR (TMTF) SPONSORSHIP PACKAGES September 11, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Zaidi ya Milioni 293 za RUWASA Zawatua Ndoo Kichwani Wananchi 10,448 Nzera&Bugando

    March 19, 2023
  • Tupeleke Mafunzo ya Mfumo wa PVMIS Ngazi za Vituo- Asema Dkt.Mkapa

    March 16, 2023
  • Mfumo wa PVMIS Kurahisisha Upatikanaji wa Bidhaa za Afya-Geita

    March 14, 2023
  • Mfumo wa PVMIS Kurahisisha Upatikanaji wa Bidhaa za Afya-Geita

    March 14, 2023
  • Tazama Zote

Video

Mwaliko Jukwaa la Fursa za Biashara Mkoani Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa