• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mamlaka za Serikali za Mitaa
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Geita Dc Yaja Kivingine, Sekondari Mpya Kuanzishwa Kama Uyoga.

Posted on: April 17th, 2021

Kiitikio cha salamu mpya hapa nchini Tanzania kijulikanacho kama “kazi iendelee” kimeendelea kudhihirika mkoani Geita Aprili 17, 2021 baada ya mkuu wa mkoa wa Geita mhandisi Robert Gabriel kuweka mawe ya msingi katika shule za sekondari mpya tatu za Izumacheli, Mnyala pamoja na Katoma kati ya zinazoendelea kujengwa ndani ya halmashauri ya wilaya ya Geita, jimbo la Geita ikiwa ni jimbo la sita kutembelewa katika ziara yake kuyatembelea majimbo saba ya mkoa mzima.

Katika ziara yake, mhandisi Gabriel ameeleza kufurahishwa kwake kwa hatua ya ujenzi iliyofikiwa kwenye shule hizo na kuahidi kuwa, kwaiba ya serikali atahakikisha anaendelea kuunga mkono jitihada zilizooneshwa na wananchi, wadau pamoja na halmashauri katika kuongeza miundombinu ili kuwasaidia wanafunzi ndani ya kata zao, huku akiwakumbusha wadau mbalimbali wa maendeleo ndani ya Geita kuikumbuka kata ya Izumacheli ambayo ipo ndani ya kisiwa lakini pia kuutaka uongozi kuweka jitihada kumalizia madarasa yaliyobaki na kuanza ujenzi wa mabweni pamoja na maabara.

“hii ni ziara yangu kwa mkoa mzima, nimefarijika sana kwa jinsi mnavyojituma kufanya kazi. Pongezi kwenu kampuni za African Underground Mining Services ltd, AKO Group Ltd, Eagle Brand Mining ltd, na Capital Drilling bila kumsahau mbunge Joseph Musukuma kwa kuunga mkono juhudi za serikali na wananchi katika kujiletea maendeleo, hivyo na makampuni mengine Geita muikumbuke Izumacheli na shule nyingine pia” alisema mhandisi Gabriel.


Akihitimisha ziara yake, mhandisi Gabriel amewataka wazazi wawahimize watoto wao kusoma ili siku moja kata zao zitoe viongozi bora wa kuliongoza taifa lakini pia kama mkakati wa kuondoa umasikini kwenye jamii huku akiwaasa viongozi kuacha alama na siyo lawama, wakileta matokeo na siyo matukio.

Wananchi wa kata ya Izumacheli ambacho ni kisiwa nao wakaiomba serikali kuona namna bora ya kuwasaidia upatikanaji wa maji safi na salama ukizingatia uwepo wa wanyama hatari “Mamba” kwenye mwambao wa ziwa wanalolitumia kupata maji, kuwawezesha vyombo vya usafiri majini ili iwasaidie kupunguza gharama ya vifaa vya ujenzi lakini pia ujenzi wa bweni kuepuka wanafunzi kuvuka maji kila watakapoenda shule.

Kwa upande wa kata ya Nkome na Katoma zilipo shule za Mnyala na Katoma sambamba, wameiomba serikali kuzisaidia umeme pamoja na maji safi na salama, suala lilitolewa ufafanuzi na wataalamu wa maji na umeme kwa kuhakikisha kuwa, umeme utayafikia maeneo hayo kuanzia mwezi Julai, 2021 na maji kupatikana kupitia mradi mkubwa wa maji utakaotekelezwa hivi karibuni.

Katika ziara hiyo iliyohudhuliwa na viongozi wa tarafa na kata, wa chama tawala CCM na serikali, mhandisi Gabriel aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Geita Fadhili Juma, mkurugenzi wa halmashauri,  wataalam wa sekta ya elimu, afya, maji, umeme na mipango ngazi ya mkoa na wilaya ambao waliweza kutolea ufafanuzi masuala mbalimbali yaliyojitokeza kwenye ziara hiyo.



Matangazo

  • WALIOCHAGULIWA MAFUNZO YA KILIMO KUPITIA PROGRAMU YA BBT-YIA FEBRUARI, 2023 March 16, 2023
  • KARIBU UPATE FOMU YA USHIRIKI KWENYE MAOENSHO YA TANO YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI 2022 September 11, 2022
  • THE 5TH TANZANIA MINERALS TRADE FAIR (TMTF) PARTICIPATION FORM September 12, 2022
  • THE 5TH TANZANIA MINERALS TRADE FAIR (TMTF) SPONSORSHIP PACKAGES September 11, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Zaidi ya Milioni 293 za RUWASA Zawatua Ndoo Kichwani Wananchi 10,448 Nzera&Bugando

    March 19, 2023
  • Tupeleke Mafunzo ya Mfumo wa PVMIS Ngazi za Vituo- Asema Dkt.Mkapa

    March 16, 2023
  • Mfumo wa PVMIS Kurahisisha Upatikanaji wa Bidhaa za Afya-Geita

    March 14, 2023
  • Mfumo wa PVMIS Kurahisisha Upatikanaji wa Bidhaa za Afya-Geita

    March 14, 2023
  • Tazama Zote

Video

Mwaliko Jukwaa la Fursa za Biashara Mkoani Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa