• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mamlaka za Serikali za Mitaa
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Chanjo ya Uviko 19 (Covid 19) yazinduliwa Geita

Posted on: August 4th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Rosemary Senyamule amewaongoza wananchi wa Mkoa huo kupata Chanjo ya Ugonjwa wa Uviko 19 (Covid 19) leo tarehe 04 Agosti, 2021 kwenye hafla fupi ya uzinduzi iliyofanyika kwenye Ukumbi wa GEDECO mjini Geita.


Akizungumza kwenye Uzinduzi huo Mhe. Mkuu wa Mkoa ameishukuru serikali kwa kuwajali wananchi kwa kuwaletea Chanjo ili kuwakinga na Maradhi hayo yaliyo kwenye wimbi la tatu la maambukizi tangia kuibuka kwa ugonjwa huo mwaka 2019. 


Aidha, Mhe. Mkuu wa Mkoa ametoa rai kwa wananchi kwenda kupata Chanjo hiyo kuanzia leo siku ya uzinduzi kwenye vituo vilivyobainishwa ambapo kwa Mkoa wa Geita wananchi wapatao elfu 50 watapata Chanjo hiyo kwa awamu ya kwanza kwenye vituo 18 yaani vituo vitatu kwenye kila Wilaya.


"Serikali yangu inajali na inawatakia mema watanzania wote, natoa wito kwa Makundi yote yaliyobainishwa kwa awamu ya kwanza kwenda kupata chanjo hii muhimu", amesema.


Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe. Wilson Shimo pamoja na mambo mengine ametoa rai kwa wananchi kufanya mazoezi ya viungo na kuzingatia Lishe Bora kwa kula vyakula vyenye mlo kamili pamoja na vitamini C.


"Tunachokifanya hapa ni kwa maslahi ya Afya zetu, ..twendeni tukapate chanjo kwani pamoja maneno mengi yanayozunguka lakini hili tatizo lipo". amesema Mwinyiheri Baraza, kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi Mkoa.


Askofu wa Kanisa katoriki Mkoa wa Geita, Flavian Kasala ametoa pongezi kwa serikali kwa uamuzi wa kuwapatia Chanjo ya Ugonjwa wa Uviko 19 ( Covid 19) na amewasihi wananchi kupata Chanjo ya Ugonjwa ili kulinda Afya zao. "katika awamu hii ya mzunguko wa tatu, tatizo hili limejidhihirisha kuwa ni kubwa sana," amesema.


"Ni nafasi kwa sisi kuonesha Imani kubwa kwenu katika kutusimamia kwani uwepo wenu ni kwa ajili ya Ustawi wa Taifa, kwani utaalamu wa kisayansi na Imani kwa viongozi wetu Mimi binafsi nakubali kuingia katika Chanjo na natoa wito kila mmoja ajitafakari na aone umuhimu na kupata Chanjo". Askofu Kasala.


Mganga Mkuu wa Mkoa wa Geita Japhet Simeo amebainisha kuwa Chanjo ya ugonjwa wa Uviko 19 (COVID 19) inasaidia kupunguza uwezekano wa mgonjwa kupata dalili kali na hatarishi na inapunguza upotevu wa uhai wa watu. Aidha, Mganga Mkuu amesema Mkoani Geita jumla ya wananchi laki tatu watapata Chanjo hiyo.


Matangazo

  • MATOEKEO YA KIDATO CHA SITA YATANGAZWA July 05, 2022
  • HOTUBA YA BAJETI YA NCHI KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2023 June 01, 2022
  • BAJETI YA MKOA June 28, 2022
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan Amemuapisha Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Rosemary Staki Senyamule Tarehe 19 Mei 2021 May 19, 2021
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • “Watumishi Jipangeni Kuwahudumia Wananchi, Ofisi Tunayo”- Asema RC Shigela

    August 06, 2022
  • “Sensa ni Kipaumbele Chetu Hadi Agosti 23, 2022”. Asema RC Shigella.

    August 05, 2022
  • “Sensa ni Kipaumbele Chetu Hadi Agosti 23, 2022”. Asema RC Shigella.

    August 05, 2022
  • Sensa si Mzaha, ni Maisha ya Watu, Tujiandae Kuhesabiwa-Asema RC Senyamule

    July 28, 2022
  • Tazama Zote

Video

Mwaliko Jukwaa la Fursa za Biashara Mkoani Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa